MUNGU WETU NI MOTO ULAO WAEBRANIA 12:29.

Saturday, September 11, 2010

GET TOGETHER PARTY IN PARADISE CITY HOTEL

Hii ndo Eid ya kipekee ndani ya kiota cha maraha paradise , kiukweli ilipendeza sana na kuvutia kwa wingi na watu walikunywa kula kasoro kulala ilikuwa raha juu ya raha na yote haya yalifanywa kwa upendo wa hali ya juu na Manager Director wa Paradise City All suite hotel and conference centre kusema kweli ni upendo wa ajabu ambao kwa mtazamo wa kibinadamu uwezi kuuona na wala kuujua kwa ukaribu ila yeye aliyetuumba anajua upendo wa director huyo ukoje


Ilikuwa ni eid get together staff party ndani ya ukumbu mkubwa kabisa humu humu ndani Serengeti ball room ukumbu ilipambwa ukapambika na team zima ya meneja wote wa paradise huku swala nzima likiongozwa kwa karibu na meneja mwajiri


Tuliamua kufanya kitu special namna hiii kiukweli ukumbi ulipendeza kama kuna harusi vile

 Vyakula vilikuwa vyakutosha kabisa kiukweli Chef anastahili sifa kwa hili

Chef mkuu Mr Ramadhani alionyesha upendo wa pekee kwa Staff wake
Kila mtu alikuwa na furaha ya kipekee kwani hakuna aliyeamini kuwa msosi ungekuwa mtamu kiasi hiko na tena kula kwa pamoja kama ndungu mmoja

Wakati watu wanapata mbili tatu burudani ilikuwa inaongozwa na band maharufu sanaaa Babiloon band mambo yalikuwa si yakawaida kabisa hapa ndani ya serengeti ball room
Bar Lady alijipanga vyakutosha hivyo ni baadhi ya vinywaji ambavyo anasema vilikuwa vinapatikana kwa wingi kabisaaaaa si mwingine ni Sweeetyy

Tulisahau matatizo yetu kisha kwa furaha tukashea mawazo

Leo ilikuwa ni zamu ya mameneja kusarve mambo yalikuwa mazuri kupita kiasi

"lema nakuambia pelka haya maji usintanie mimi nshazoea kubeba mafaili ni upendo du unanifanya nifanye haya yote " Thank u dada Lidya alikuwa bega kwa bega kuakikisha mabo yanakwenda sawa sawa
Hatukuishia hapo tu watu walipongezwa kwa zawadi na vyeti ilikuwa ni furaha ya kipekee aswa pale mtu au kundi la watu wanapokubali kile ambacho unafanya Picha juu dada yangu mpendwa Hellen akipongezwa kwa zawadi

Dada Asha ni mmoja kati ya wale walio pewa zawadi kwa kazi nzuri kabisa walio ifanya hapa paradise city hotel
Nami nilikuwa mstari wa mbele jamani sikukosa zawadi kabisa


Huyu ni moja kati ya watu ambao kwangu mimi ntazidi kuwapa heshimi kwa ajili ya kitu kimoja kwanza ni mvumilivu pili ni mchapa kazi tatu analongolongo na mtu na mwisho kabisa anaupendo wa hali ya juu kwa wale anaowaongoza si mwingine ni Brother Ramadhani au Baba Ronaldooooooooo
Baiyaaaa u rock naaaaaaa naye alipokea cheti
Kiukwli mambo yalikuwamazuri na watu walifurahi kama hivi


General manager akifanya mabo yake ya ngwasuma ha ha ha ha raha juu ya raha
 Huu ni upendo wa hali ya juu walioonyesha mameneja wa Paradise all suite hotel

Napenda niwashukuru wote kwa upendo wao na ukarimi lakini fursa hii pia napenda kuichukua kwa kumshukuru MD kwa kutupa uwezo wa kufanya haya yote ninachosema hatuna cha kumlipa ila Mola atazidisha pale alipotoa patajazwa kiasi cha kusukwa sukwa

 Napenda niseme maneno haya najua yatafika kwako tu tazama ulivyowakusanisha ndugu kwa pamoja tena kwa upendo nadhani umetimiza maandika yaliyoandikwa katika zaburi

Lema one and my MD Mr JB

Behold, how good and how pleasant it is for brethren to dwell together in unity!It is like the precious ointment upon the head, that ran down upon the beard, even Aaron's beard: that went down to the skirts of his garments; As the dew of Hermon, and as the dew that descended upon the mountains of Zion: for there the LORD commanded the blessing, even life for evermore.


HAYO NDO MAMBO YA PARADISE CITY HOTEL 

1 comment:

Anonymous said...

wao mko juu kaka lema one mabo yenu mazito kaka yaani mpaka band humo humo kaka nipatie email adress ya kwako binafsi nitakuinbox