MUNGU WETU NI MOTO ULAO WAEBRANIA 12:29.

Thursday, September 30, 2021

NGUVU YA MSAMAHA*



_*Na Bishop Danktin Rudovick Rweikila*_


*18th August 2021*


Mathayo 6:9-15

_*[9]Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje,

[10]Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.[11]Utupe leo riziki yetu [12]Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu. [13]Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.] [14]Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.[15]Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.*_


Katika maombi haya hakuna mhali Yesu alipoweka sharti isipokuwa kwenye mstaru wa kumi na mbili. Mstari hu9 ndiyo ambao una sharti la wewe kusamehe. Makosa yako yanafutwa na nguvu ya msamaha. Kama unavyoonyesha kuwasamehe waliokukosea ndivyo unapata nafasi ya msamaha. KAMA HAUNA NEEMA YA KUSAMEHE KWENYE NYAKATI HIZI ZA MWISHO MLANGO WAKO WA KWENDA MBINGUNI UMEFUGWA. 


Yesu alikuja kukomboa ulimwengu baada ya Mungu kutusamehe, huu msamaha unawahusu wale ambao wanasamehe. Kila mmmoja anatamani msamaha na tunaenda mbele za Mungu kuomba msamaha. Ni maumivu makubwa sana na hauwezi kusamehe pasipo kuondoa yale maumivu ya makosa uliyokosewa. 


Tumeacha vyote kwaajili ya Kristo ili tuweze kupata ufalme wa mbinguni. Tumepata Neema ya kuokolewa na tunapezwa usiku na mchana na kuonekana wajinga kwasababu ya kuutafuta ufalme wa mbinguni. Haya yote yamebebwa na nguvu ya msamaha. Pasipo kusamehe iwe unajitoa kwenywe kazi ya Mungu kwa nguvu sana lakini unahitaji kusamehe. 


Toba haina maana kwako kama wewe unayeomba haujasamehe waliokukosea. Ndiyo maana Biblia inasema usipowasamehe watu makosa yao Baba wa mbinguni hawezi kukusamehe. 


Sasa utajuaje umesamehewa? 


*Mathayo 7:15-20*

_*[15]Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali. [16]Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? [17]Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya. [18]Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. [19]Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni. [20]Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.*_


Huu ndiyo udhuhirisho wa wateule siku hizi za mwisho. Si vazi la kujificha kwenye kanisa la walokole haitakusaidia ni ile hali ya kumaanisha. Kubadilishwa kwa ndani. Matunda yako yatakutambulisha. 


Ile hali ya kwamba huko kwenye kanisa la kilokole lakini ndani umejaa umbea, huzushi n.k. Wakati unakuja ambao hautaweza kuomba pasipokuwa na utakatifu. Kuna neema ilikuwa inaendelea kwetu ili tuifanye kazi ya Mungu. 


Matunda mabaya ni muonekano wako, matendo yako, tabia zako n.k, mti mwovu hauwezi kuzaa matunda mema. Na Yesu anasema kila mwenye matendo mabaya anakatwa na kutupwa motoni. Tunafunga na kuomba si ili tupate pesa bali tupate ufalme wa mbinguni. 


Ni majira ya kujiandaa kwa kanisa maana Bwana harusi anakuja saa yeyote katika nyakati hizi. 



Sunday, March 28, 2021

♨♨ KUSHINDANA NA ROHO YA FARAO AU ROHO YA KIMISRI ♨♨ πŸ†•️πŸ”§


♨♨ KUSHINDANA NA ROHO YA FARAO AU ROHO YA KIMISRI ♨♨ πŸ†•️πŸ”§

28th March 2021

Na Bishop Dankton Rudovick Rweikila

Ni kweli umeomba na umevua vazi na unayo matarajio yako kwa Mungu, lakini usiposhindana roho ya farao hautaweza kutoka mahali. Roho ya Farao inatawala katika maeneo manne.

1️⃣Anga
2️⃣Ardhi
3️⃣Nchi
4️⃣Bahari

*Mwanzo 1:26-28*
_*[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. [27]Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. [28]Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.*_

Utaona namna ambavyo uliumbwa kwa mfano wa Mungu wako. Unayo nguvu ya kutawala ndani yako na umepewa akili. Wanyama wengi wana macho lakini akili hawana. Maeneo haya manne ndiyo ambayo Roho ya Farao inashughulika nayo. Ndiyo maana Farao alishindana na wana wa Israeli. Kumbuka wana wa Israeli walitaabika miaka mia nne na thelathini na walitoka ndani ya Nchi ya Misri kwa kufa wazaliwa wa kwanza tangu yule wa Farao mpaka yule wa kijakazi.wwliondoka kwa kumchinja pasaka na kuweka kwenye miimo ya milango yao na ndiyo maana Yesu alikuja kama sadaka ya Pasaka. *1 WAkorintho 5:7*

Kumbuka Farao ni mtu na ndani ya mtu kuna Roho ambayo inakaa ndani yake. Katika Nchi ya Misri walikuwa na Mungu wao ambayo ilikuwa ni Roho za mashetani.

*Isaya 19:3*
_*[3]Na roho ya Misri itamwagika kabisa katikati yake, nami nitayabatilisha mashauri yake, nao watakwenda kwa sanamu zao, na kwa waganga, na kwa wapiga ramli, na kwa wachawi.Unaweza kushangaa ndani ya familia kuna watu ambao hawamtambui Mungu kwasababu wanakuwa na hii roho ya kimisri, utakutq mtu yuko tayari kwenda hata nje ya anchi kwasababu ya waganga wa kienyeji lakini kuja kanisani mtu ataki ni kwasababu ya hii roho ya kimisri. Sasa usishindane nao bali shindana na hii roho ya kimisri.*_

Roho ya Farao maana yake nini?

1️⃣ _Ni roho ya kuua kila kichanga au hatua yako ya kwanza unayoanza kwenye maisha yako._

Farao anasubiri unapata kazi na unapooanza siku ya kwanza wanaanza ugomvi na wewe na unashangaa mbona nachukiwa bila sababu, roho hii inaua nia ya kwanza na hatua ya kwanza. Wengi hii roho wanaita ya kukataliwa au ya kushindwa.

*Kutoka 1:15-16*
_*[15]Kisha mfalme wa Misri akasema na wazalisha wa Waebrania, mmoja jina lake aliitwa Shifra, na wa pili jina lake aliitwa Pua [16]akasema, Wakati mwazalishapo wanawake wa Kiebrania na kuwaona wa katika kuzaa, ikiwa ni mtoto mwanamume, basi mwueni, bali ikiwa ni mtoto mwanamke, na aishi.*_

Farao alipoona Waebrania wanaongezeka kwa maana wana matarajio ya kutoka Misri akainuka kinyume nao. Roho ya Farao inaanza kuona matarajio yako ambayo unayo ndani yako kwamba utaanza kutoka utumwani. Mtu anayo matarajio ya kupata kazi Faraonanaanza kuharibu kwenye chanzo na kuua mahusiano. Farao alipoona wanaongezeka akaongea na wazalisha kwamba kila mwanaume anayezaliwa hauwawe. Maana yake kila biashara inayozaliwa kwako ife, kila mtaji unaopata ufe.

Leo nimekuja na ile sauti ya Musa kwaajili ya kila mtu ambaye anateswa na Roho hii ya Farao kwa jina la Yesu Kristo wa Nazarethi.

Adui yako lazima ashirikiane na waganga wa kienyeji na wachawi sasa sikiliza ukiona hii roho inanguvu geuza wale waliotumwa ili washirikiane na madhabahu ya Mungu wako. Lazima uende kwa ufunuo geuza mioyo yao wawe wachaMungu. Wale wazalisha walipopewa agizo hawakuweza kugusa watoto wa kiebrania. Wakasema kabla ya sisi kuwazalisha tunakuta wamezaa wenyewe.

Sikia neno la Bwana waebrania siyo kama wamisri hawasubiri kupewa mitaji bali tunapoenda tunawakuta na mitaji na hatujui wametoa wapi? Walisema ikiwa ni biashara yenye faida ikiwa ni ndoa yenye amani hakikisha imeua. Ukiona mtoto wake anayo matarajio ya kuwa waziri hakikisha mmeua. Ukiona mtu anatoa sadaka na inaleta matokeo hakikisha mmeua. Waliambiwa wakiona Muebrania ni mjamzito wafuatilie kwamba ni kitu gani kitazaliwa. Wanasema haya maombi anayoomba yakufunga yanamatokeo sawa mpe usingizi, je ibada anazokwenda zinamatokeo mpe kazi nyingi na ubize ili kiroho chake kipoe na maono yapotee.

*Maombi*

Kuanzia leo ninaikataa hii roho ya kafao haitanizuia kwa jina la Yesu

Elewa jambo moja mwembrania hataelewa ni kwanini mtoto amekufa atajua ni bahati mbaya au ni kawaida tu. Yaani biashara kufa unaona kawaida tu kumbe ni hii Roho ya Farao.

*Omba maombi haya*

Bwana Yesu ninaifuta hii roho juu yangu roho ya farao ninaikataa iliyonitaabisha miaka mingi ninaondoa kwenye familia yangu kazi yangu kwenye uchumi wangu ninaondoa kuanzaia leo kwa jina la Yesu. Wewe anga achia wewe bahari achia wewe ardhi achia kwa jina la Yesu malango ya mzaliwa wa kwanza achia kwa jina la Yesu Kristo wa Nazarethi.

2️⃣ _Roho ya Farao inakutumikisha kwa kazi ngumu na yenye mateso kwa muda mrefu bila faida._

Unafanya kazi kwa nguvu tena ngumu na unachelewa kulala ukiandika mipango na Diary inajaa lakini hakuna hata mpango mmoja uliofanikiwa. Unachlewa kurudi nyumbani hata majirani hawakujui lakini jirani yako anakuja saa kumi na moja anayo matokeo chanya. UmeΓ jiriwa kwenye kiwanda miaka nenda rudi lakini hauna faida umebakia kuwa mtumwa tu.

*Kutoka 14:5-6*
_*[5]Mfalme wa Misri aliambiwa ya kuwa wale watu wamekwisha kimbia; na moyo wa Farao, na mioyo ya watumishi wake, iligeuzwa iwe kinyume cha hao watu, nao wakasema, Ni nini jambo hili tulilotenda, kwa kuwaacha Waisraeli waende zao wasitutumikie tena [6]Akaandalia gari lake, akawachukua watu wake pamoja naye;*_

Roho ya Farao haiwezi kukuruhusu kutoka tu. Walipoona wametoka walikaa kikao wakasema kwanini tumewaruhusu hawa watu kutoka. Alipigwa kwenye ibada na akatoka alafu unafika nyumbani wanasema imekuwaje tumemruhusu huyu mtu kutoka. Sasa kwasababu wamezoea kutumia akili zako, kichwa chako wataanza kuuliza kwanini tumeruhusu. Ndiyo maana unakuwa na ushindani hata kuja ibadani. Mungu alishuka na kugeuza moyo wa Farao uwe mgumu na akawafuatia *USIOGOPE WANAKUFUATIA KWA JINA LA YESU.*

Wana wa Israeli walitembea kwa miguu na walipotoka Farao akaandaa gari lake ili kuwafuatia, yaani umetaabika muda mrefu lakini siku moja tu roho hii i akuangusha. Usipomtegemea Mungu hii roho ya Farao ni siku moja itakurudisha nyuma. Roho ya Farao inakurudisha haraka chini kuliko ulivyoenda. Farao alichagua magari mia sita ili kuwafuatia na kuwarudhisha kwa siku moja.

Walipoanza kisogea wana wa Israeli wakaanza kutetemeka. Usitawaliwe na Roho ya hofu kwasababu itakurudisha utumwani. Nyuma ya Roho ya hofu kuna Roho ya Farao. Ujawahi kuona umegoma kwenda kanisani na mtu akikuuliza hauna sababu ya kusema. Roho ya Farao inakuonyesha umauti kabla ya kufa inakuonyesha umasikini kabla haujakupata inakuonyesha kushindwa kabla ya kushindana. Hii roho inakufanya uache kazi kabla ya kuandikiwa barua. Wana wa Israeli walisahau mkono wa Bwana uliowatetea kwa mapigo kumi na wakatoka misri walimnungunikia Musa lawama zikaanza kutawala. Wale walimungunikia Musa inawezekana na wewe kuna uliowalaumu kwasababu ya kushindwa kwako na ukawalaumu kweli sikiliza usiangukie mtu ukafikiri yeye ndiye amekufanya kushindwa. Kila aliyeshindwa anasababu zankushindwa lakini nakutangazia leo ukashinde katika jina la Yesu Kristo.

Wanamuambia Musa neno hili silo tulilokuambia tukiwa Misri kwamba utaondoka na Farao atatufuata, waliondoka wakiwa na matarajio ya kurudishwa lakini Musa yeye akulia wala kutarajia kurudi Misri. Musa aliwaambia watu hivi, *_Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele._*

Furaha nyingine ni hii kwamba hautatoka kwa Farao mikono mitupu

Kutoka 3:6-7

3️⃣ Roho ya Farao inakuweka utumwani muda mrefu

Biblia inasema Roho ya Farao iliwaweka miaka 430 wana wa Israeli UTUMWANI. Sijajua wewe umekaa na huo ugonjwa kwa miaka mingapi, sijajua miaka yote nini kinakutesa hiyo ni roho ya Farao lazima ugeuze maombi yako na kuanza kupiga Roho ya Farao. Kila mlango unaotokea unazuiliwa hii ni Roho ya Farao. Miaka mia nne wana wa Israeli wanalia kwa utumwa. Sijajua ninmuda gani unaomba na haujafanikiwa hiyo ni Roho ya Farao.

Maombi
Bwana Yesu kuanzia leo naikataa Rho ya Farao inayotenda kazi kupitia anga kwa jina la Yesu Kristo wa Nazarethi. Endelea kuomba kwa ajili ya kila eneo ambalo umekaa muda iwe ni biashara haina matunda muda mrefu, ndoa, kazi, magonjwa ya muda mrefu piga kwa jina la Yesu Kristo wa Nazarethi ili viachie maisha yako. Achilia moto kwenye anga, achilia moto ulao kwenye ardhi baharini mimina moto wa damu ya Yesu.

*Kutoka 12:40-42*

_*[40]Basi wana wa Israeli kukaa kwao, maana, muda waliokaa ndani ya Misri, ulikuwa ni miaka mia nne na thelathini. [41]Ilikuwa mwisho wa miaka hiyo mia nne na thelathini, ilikuwa siku ile ile, ya kwamba majeshi yote ya BWANA yalitoka nchi ya Misri. [42]Ni usiku wa kuangaliwa sana mbele za BWANA kwa sababu ya kuwatoa katika nchi ya Misri; huu ndio usiku wa BWANA, ambao wapasa kuangaliwa sana na wana wa Israeli wote katika vizazi vyao.*_

Walitumikishwa miaka 430 na Bwana alikaa kimya lakini wakati ulipofika hawakutoka watupu na wewe leo unayesoma haya na kuomba maombi haya hautatoka mtupu. Walizuianuzao wako utapata mapacha mpaka useme Bwana yatosha, walizuia amani yako utakuwa na amani mapaka wakushangae, walikuzuia usiolewa utaolewa na harusi yako itakuwa ya maajabu, walikuzuia usipande cheo utapanda mara mbilli kwa jina la Yesu. Haya si maneno yangu ni Bwana anasema _*Nami nitawapa watu hao kufadhiliwa mbele ya Wamisri; hata itakuwa, hapo mtakapokwenda zenu hamtakwenda kitupu;*_ *Kutoka 3:21* Hao waliokataa kukusaidia muda wote watageuka na kuanza kukusaidia wewe hao ambao walikutisha Bwana atawageuza kuwa msaada kwako. Kabla hawajapigwa kwanza wakusaidie alafu kisha watapigwa.

Mungu ni waajabu endelea kumtegemea na kumtafuta hata kama ni miaka kumi si wamekuona unamuimbia Yesu na wao wakashughulikia maisha yako wakati wanalia wewe utakuwa umeketi na wafalme.

Ngoja nijaribu hivi najua utaelewa

Wakati unaita nyota yako haitarudi kitupu bali itarudi na gari lako. Yule ambaye alikufunga akawa na nyumba u apofunguliwa utanunua na nyumba yake. Yule aliyechukua akili yako ukafeli na ukarudia madarasa yeye ameajiriwa na wewe ndo umemaliza elimu sasa hivi sikiliza neno la Bwana wewe unayesoma haya na kuomba utabeba cheo chake yeye. Unaweza kusema Bishop neno ili linakuwaje, Mordekai alikuwa akikaa malangoni na mtumwa tu lakini ghafla Hamani aliyekuwa anataka afe kibao kikageuka. Walikuwa wamepanga mabaya jΓΉu ya Mordekai. Hamani wakati anaulizwa alijua ni yeye kumbe majira yalikuwa yamebadilika.

*Esta 6:1-10*
_*[1]Usiku ule mfalme hakupata usingizi; akaamuru aletewe kitabu cha maandiko ya taarifa, nayo yakasomwa mbele ya mfalme [2]Ikaonekana kuwa imeandikwa ya kwamba Mordekai aliwachongea Bigthana na Tereshi, wasimamizi wawili wa mfalme, katika hao waliolinda mlango, waliotaka kumtia mikono mfalme Ahasuero. [3]Mfalme akasema, Je! Ni heshima gani au jaha gani Mordekai aliyofanyiziwa kwa ajili ya hayo? Watumwa wa mfalme waliomhudumu wakamwambia, Hakuna alilofanyiziwa. [4]Mfalme akasema, Yupo nani behewani? Ikawa Hamani alikuwa ameingia katika ua wa nje wa nyumba ya mfalme, aseme na mfalme, ili kumtundika Mordekai juu ya mti ule aliomwekea tayari. [5]Basi watumwa wa mfalme wakamwambia, Tazama, Hamani yupo, amesimama behewani. Mfalme akasema, Na aingie. [6]Basi Hamani akaingia. Mfalme akamwambia, Afanyiziwe nini yule ambaye mfalme apenda kumheshimu? Hamani akasema moyoni mwake, Ni nani ambaye mfalme apenda kumheshimu kuliko mimi? [7]Basi Hamani akamwambia mfalme, Yule ambaye mfalme apenda kumheshimu, [8]na aletewe mavazi ya kifalme ambayo mfalme amezoea kuyavaa, na farasi ambaye mfalme humpanda mwenyewe, ambaye ametiwa taji ya kifalme kichwani; [9]na yale mavazi na yule farasi akabidhiwe mkononi mmojawapo wa maakida wa mfalme aliye mstahiki; ili makusudi amvike yule ambaye mfalme apenda kumheshimu, na kumrakibisha juu ya farasi kuipitia njia kuu ya mjini, na kupiga mbiu mbele yake, kusema, Hivyo ndivyo atakavyofanyiziwa mtu yule ambaye mfalme apenda kumheshimu. [10]Basi mfalme akamwambia Hamani, Hima! Twaa mavazi na farasi kama ulivyosema, ukamfanyizie vivyo hivyo Mordekai, Myahudi, aketiye mlangoni pa mfalme; lisipungue neno lo lote katika yote uliyoyasema.*_

Mordekai alisimamiwa na mfalme na alikupungua neno hata moja. Na leo mbingu inakusimamia alitapungua hata neno moja watarudisha vyote, kazi yako, kipawa chako, ndoa yako, mume wako, mke wako, watoto wako kwa jina la Yesu Kristo wa Nazarethi. 

Thursday, March 25, 2021

ⓂⒶⓉⒶⓇⒶⒿⒾⓄ ⓎⒶⓀⓄ 3 *MATARAJIO YAKO* 3

 


ⓂⒶⓉⒶⓇⒶⒿⒾⓄ ⓎⒶⓀⓄ 3 *MATARAJIO YAKO* 3

25𝓽𝓱 π“œπ“ͺ𝓻𝓬𝓱 2021

Tunaendelea katika hatua ambazo tulianza jana za _Ufanye nini ili matarajio yako yapate kutimia au yaendelee kuwepo_*❓

3️⃣ MALANGO

Nilisema unaweza kuwa mtumishi lakini usiweze kuingia kwenye malango ya utumishi, Biblia inasema anasimama mlangoni na anabisha hodi. Unapoona unamatarajio ambayo hayatimii tazama lango lako la Baraka ili uweze kuingia.

Sasa ninaenda kwenye somo ili kwa mtiririko ufuatao,

*Jambo la kwanza*

_Shukrani_

Shukurani maana yake ni kuamini umetendewa na ni vyakako. Unapokuwa kwenye maombi elewa unachoomba kwasababu malango yanaweza kuwa wazi. Kwenye Biblia utaona watu walifunga na kuomba lakini hawakuwa na matarajio kwamba wanaweza kupata walichoomba. Mungu anaweza kukupa kile ulichoomba na ukakataa.

*Matendo ya Mitume 12:12-17*

*_[12]Na alipokuwa akifikiri haya akafika nyumbani kwa Mariamu, mamaye Yohana, ambaye jina lake la pili ni Marko; na watu wengi walikuwa wamekutana humo wakiomba. [13]Naye alipobisha kilango cha lango, kijakazi, jina lake Roda, akaja kusikiliza. [14]Alipoitambua sauti ya Petro, hakukifungua lango, kwa ajili ya furaha, bali alipiga mbio, akaingia ndani akawaambia kwamba Petro anasimama mbele ya lango. [15]Wakamwambia, Una wazimu. Lakini yeye akakaza sana, akasema ya kwamba ndivyo hivyo. Wakanena, Ni malaika wake [16]Petro akafuliza kugonga, hata walipokwisha kumfungulia wakamwona, wakastaajabu. [17]Naye akawapungia mkono wanyamaze, akawaeleza jinsi Bwana alivyomtoa katika gereza. Akasema, Kampasheni Yakobo na wale ndugu habari hizi. Akaondoka, akaenda mahali pengine._*

Unaweza kufurahi lakini usifungue malango yako na muujiza wako ukabaki nje ingawa unausikia.

Wakati kijakazi anafurahi tuchukulie kwamba maaskari wangemkuta nje na Roda alikuwa ajafungua mlango. Angalia huu ni muujiza wako umetokea na umeuacha nje tu kwasababu umefurahia. Usiishie kufurahi bali fungua malango ili muujiza wako usipotee. Kumbuka wale wanafunzi walirudi wakifurahi na Yesu aliwaambia msifurahie utumishi huo lakini wafurahi kama majina yao yameandikwa mbinguni.

Walimuambia kijakazi ana wazimu kwa maana walikuwa hawana imani na kile walichokuwa wanaomba. Ndiyo maana walimuambia Kijakazi unawazimu wewe. Umeomba kupata mtaji na unapopata unasema sina biashara uliomba lakini haukuwa na matarajio ya kupata. Huyu ni Petro amekataliwa na bado amengangana mlangoni je muujiza wako utaendelea kugonga mlangoni. Unasikia kuombq kwaajili yq huduma yako lakini Mungu anapoachilia wingu la kwenda mahali unakataa sasa uliomba ya nini ?. Unaomba moto wa maombi unasikia mfungo wa siku 40 alafu unanuna sasa uliomba nini maana Mungu anataka ndani ya siku 40 moto ukamate.

Yule kijakazi walimuita mwendewazimu sasa kati ya wao na kijakazi nani alikuwa mwendewazimu. Kijakazi alipokaza kusema wakasema ni malaika wa Petro ni kweli malaikq wa Petro alimtoa gerezani lakini akuendelea kuonekana bali Petro ndo alionekana. Sijajua ni wangapi umefukuza na kuwaita wendewazimu. Hawa ndugu wamejifungia na wanaomba lakini imani ya kiwa yatakuwa yao haikuwepo. Kijakazi mwenyewe anaanza kushuhudia kabla ya kifungua mlango jaribu kufikiri wangefika pale wale askari ushuhuda ungepotea wa Roda. Ndivyo walokole walivyo wanaanZa kutangaza mafanikio yao kabla ya kufungua malango. Walianza kugeuza matarajio yake wakasema uu mwendewazimu kwasababu haujui kutofautisha kati ya Petro na Malaika wake.

Petro alifululiza kupiga kelele mlangoni hata walipokuwa wakishauriana ndani. Sikiliza muujiza wako hata wasemeje utaendelea kupiga kelele mlangoni.

Walistaajabu !!!!!!

Kwanini hawa ndugu walistaajabu ni baada ya kumuona Petro aliyekuwa mlangoni. Sikia watakapoona unainuliwa acha wastaajabu walikuona mjinga na mwendewaZimu lakini Bwana atakapoinuka na kuanza kukubariki wacha wastaajabu. Katika siku nilizotamka 90 wacha maadui zako wastaajabu, walikuona wakawaida na ukadhalilika lakini natangaza miezi mitatu wastaajabu na neema ya Bwana iwe juu yako. Uwe mtu mwingine kama ambavyo Farao alistaajabu kwa Waebrania wakati wakiondoka Misri wakiwa na vitu.

Tukimaliza hili somo nitakuonyesha hii Roho ya Farao na utaona viti ambavyo vimebebwa na hii roho ya Farao. Roho ya kutokumcha Bwana ni roho ya kimisri, nitakuja kukuonyesha. Wana wa Israeli walikuwa na matarajio yao lakini walipoingia misri wakawa watumwa na Mungu aliwaokoa kwenye malango ya Farao. Roho ya Farao inatumikisha Waebrani na Wamisri. Umeokoka lakini Roho ya mateso iko juu yako. Ndiyo maana aliwaambia atawaokoa na magonjwa ya Misri.

*Zaburi 100:4*

_[4]Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake; Ingia malangoni kwa kushukuri_




Wednesday, March 24, 2021

 ⓂⒶⓉⒶⓇⒶⒿⒾⓄ ⓎⒶⓀⓄ ② *MATARAJIO YAKO* 2 

 ⓂⒶⓉⒶⓇⒶⒿⒾⓄ ⓎⒶⓀⓄ ② *MATARAJIO YAKO* 2 


Na Bishop Dankton Rudovick Rweikila 


24𝓽𝓱 π“œπ“ͺ𝓻𝓬𝓱 2021

*_Ufanye nini ili mztarajio yako yapate kutimia au yaendelee kuwepo_*❓

Mungu anataka vitu unavyotarajia vidhihirike.

1️⃣ Kinachoweza kuondoa matarajio yako yasitimie ni Dhambi

*Mithali 10:28*
_*[28]Matumaini yao wenye haki yatakuwa furaha; Bali kutaraji kwao wasio haki kutapotea.*_

Kinachomuondoa MUNGU kwenye matarajio yako ni dhambi. Matarajio ya mwenye haki yatatimia na inakuwa furaha. Mungu anapokutendea kuna furaha inatokea kwasababu wewe ni mwenye haki. Kuna mtu moja kwenye Biblia ambaye akujali na aliuza uzaliwa wake wa kwanza. Esau alipofika wakati wa kubarikiwa akubarikiwa kwasababu ya mambo mawili uasherati na kutokujali.

*Waebrania 12:16-17*

*_[16]Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kimoja.[17]Maana mwajua ya kuwa hata alipotaka baadaye kuirithi baraka, alikataliwa (maana hakuona nafasi ya kutubu), ijapokuwa aliitafuta sana kwa machozi._*

Esau alipopewa ile nafasi hakuithamini na ndiyo maana alipotaka kubarikiwa hata kwa machozi hakupata baraka ile. Kuna nafasi umechezea kwenye ulimwengu wa Roho kuna madhara kiasi gani? Unapokula fungu la kumi unaweza usione madhara yake lakini kuna wakati wa kubarikiwa hautapata baraka na utatafuta hiyo nafasi hata kwa machozi.

Ni rahisi kufanya biashara ukifikiri kesho utakuwa na hiyo nafasi tena na ikipotea hauwezi kuipata tena hata kwa machozi dhambi inaua matarajio ya mtu. Esau alifikiri kupewa neema ya mzaliwa wa kwanza ilikuwa ya kawaida ndiyo maana akadharau uzaliwa wa kwanza. Toba yenyewe ni neema kwasasababu Esau alitafuta lakini hakuweza. Wakati Baba yake anamtuma kwenda kuwinda ili ampikie Baba yake na kubarikiwa alikwenda akiwa na matarajio ya kupata baraka. Hakukumbuka kwamba aliuuza uzaliwa wake na hakuwahi kutubu akaona anaenda kufaulu. Lakini muda ule ule ambao alikwenda ndipo matarajio yake yaliibiwa.

Njaa ya Esau aikuwa ya kawaida bali ilikuwa ni kipimo cha yeye kumuheshimu Mungu wake. Changamoto uliyonayo ni kipimo chako cha kumuheshimu Mungu wako. Sijajua umepewa nini ndani yako lakini usidharau nafasi uliyopewa na Mungu, ukipotea utatafuta kwa machozi.

2️⃣ *_Hakikikisha unanena maneno mazuri kwa kila tukio linalotokea mbele yako._*

Maneno ni roho *( Yohana 6:63)* kwa hivyo ili kitu kife inategemeana na maneno yako. Shetani anasikiliza manenk yako na Mungu naye anasikiliza maneno yako, unaposema ndipo shetani anapata mlango wa kuyatekeleza kadhalika unaposema Mungu anaumba kupitia maneno yako. *Waebrania 11:3*

Unapotamka vyema ndipo unaachilia nuru kwa vile unavyotarajia. Ulichopewa ni faida hivyo hakikisha unatamka mema hata kama hasara inatokea wewe endelea kudai faida yako. Usigeuze matukio yasiyo ya kawaida kuwa sehemu yako. Wewe hauogozwi ma matukio bali neno la Bwana na ndilo linagengeneza picha ndani yako. Imani ni kuwa na uwakika na mambo yatarajiwayo, usiangalie mazigira au adui anayekuzunguka bali kile unafhotarajia kikupe neema ya kushinda.

*Hesabu 14:28*
_*[28]Waambieni, Kama niishivyo, asema BWANA, hakika yangu kama ninyi mlivyonena masikioni mwangu, ndivyo nitakavyowafanyia ninyi;*_

Kama ulivyosema ndivyo Bwana atakufanyia kama ukiongozwa na matukio maana yake utaongea na kunena sawa sawa na matukio ambayo yanaweza kuwa siyo matarajio yako. Unawezekana umekwama leo lakini si amarajio yako. Unapotamka kwa woga na kubeba udhahifu wa tukio ilo unalifanya liwepo.

Unapokutana na shimo siyo tukio la kukufanya ufe lakini unapotamka mabaya yataimarisha kile ulichosema kwenye kinywa chao. Mabaya hayana nguvu kama utashinda hofu ya matukio.

Changamoto zipo haijalishi huko kwenye ngazi ipi lakini changamoto ipo, mpaka utakapokwenda kwenye mji mpya na kuvumilia mpaka mwisho wake. Haushindi changamoto kwasababu umeomba leo bali ukiwa na kanuni ya Mungu utashinda changamoto. Mahesabu yanabadilika number lakini kanuni ni ile ile. Changamoto zinabadilika lakini ukijua kanuni ya Kimungu ya kutatua changamoto utashinda. Kanuni ya kwanza ya kutatua changamoto lazima umsikilize Roho Mtakatifu, yeye ndiye anajua matamanio ya Mungu wako. Yule Mama mshunami akukiri kwa kinywa chake kwamba mtoto wake amekufa na ndiyo maana Gehazi alimpomuuliza mtoto hajambo alisema hajambo *2 Wafalme 4:17-37*