MUNGU WETU NI MOTO ULAO WAEBRANIA 12:29.

Sunday, November 13, 2016

NGUZO ZA KANISA LA POWER OF GOD FIRE CHURCH WITO TULIOITIWA

Msingi katika kanisa lolote la Mungu wa kweli ni neno la MUNGU, kila kanisa la kweli lazima lianze na msingi wa neno la Mungu na siyo hisia au mapokeo ya binadamu (Mafundisho) kila kilichojengwa katika msingi imara kitadumu ndiyo maana neno la MUNGU linaitwa “mwamba” (1 Wakorintho 10:4) Yesu Kristo alifundisha kwa habari ya wajenzi wawili. Mjenzi mwenye hekima na Mjenzi Mpumbavu.

Yule mpumbavu alijenga bila msingi mvua ikaja na upepo hukavuma ukaipiga ile nyumba na ikaanguka na anguko lake ni kuu, lakini yule mjenzi mwenye hekima alijenga juu ya mwamba na mvua ikaja na upepo ukavuma, ukaipiga ile nyumba nayo ikaanguka kwa kuwa ilijengwa juu ya Mwamba. Mathayo 7:24

Hivyo kanisa ni lazima lijengwe katika msingi wa NENO kwa maana NENO ni MUNGU mwenyewe Ufunuo 19:11-13, Waebrania 11:3. Kanisa la Yesu Kristo mwenyewe kabla hajaondoka alishaweka msingi wa kanisa lake hapa duniani, kwa kusema juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu hata malango ya kuzimu ya kuzimu hayatalishinda. Mwamba huo ni KRISTO MWANA WA MUNGU ALIYE HAI Mathayo 16:18.

Hakuna Msingi mwingine zaidi ya uliowekwa na Kristo katika kanisa lake MWANA WA MUNGU aliye hai. I Wakorintho 3:11-13

IMANI WAEBRANI 11:1

      Imani ni kuwa na uhakika na mambo yatarajiwayo na ni bayana ya mambo yasiyoonekana. Msingi wa Imani ndani ya kanisa la Mungu unatokana na Neno la MUNGU ambaye ni KRISTO. Kila mwananfunzi wa Yesu yaani yeyote aliyeokolewa lazima awe na Imani juu ya wokovu alioupokea. (Yesu Kristo aliyemwamba wa wokovu) Kwa maana Imani huja kwa kusikia neno la Kristo, Warumi 10:17.

Pasipo Imani haiwezekani kumpendeza MUNGU, kwa maana kila amwendeaye Mungu lazima aamini yeye yupo na huwapatia dhawabu wale wote wampendao, Waebrania 11:6. Hivyo kanisa la Mungu lazima lijenge Imani ya waumini wake katika wokovu walioupokea sawa sawa na neno la Mungu na siyo kitu kingine. Waebrania 11:32-38, Warumi 10:11, kwa maana Mungu apendezewi na mtu au na kanisa lenye Imani ya kusita sita.  Waebrania 10:38

Hivyo ushindi juu ya Jambo lolote ni juu ya Imani yako, ndiyo maana Yesu aliwaambia watu kuwa Imani yako imekuponya

UTAKATIFU 1WAKORINTHO 3:17

Ni kanuni ambayo inatakiwa ifuatwe na kila ambaye ameokoka (Mwana wa MUNGU) kwa sababu mara baada ya kuokoka tu, Roho mtakatifu anaingia ndani yetu (Ndani ya roho zetu) na huu ndiyo unakuwa mwanzo wa nguvu za Mungu na moto wa MUNGU kushuka juu ya maisha ya mtu, kinachobaki ni kuendelea kuchochea moto huu kwa maombi na utakatifu kwa kuwa baada ya kumpokea BWANA Yesu Kristo, Roho Mtakatifu anakaaa ndani yako, na wewe unakuwa umefanyika hekalu la Mungu 1Wakorintho 3:16.

Hivyo pasipo kuchochea moto (NGUVU) wa Roho Mtakatifu moto huu utazimika “Mithali 26:20. Moto hufa kwa kukosa kuni” Kanisa la Mungu lazima likumbushwe kutunza Nguvu (MOTO) ya MUNGU kwa kukemea maovu (dhambi) na kufundisha watu kutembea katika utakatifu wote ili kulinda uwepo / Nguvu za MUNGU ndani ya Kanisa kwani nguvu za Mungu ukaa ndani yetu Waefeso 3:20, Waefeso 6:10.

UTII 1SAMWELI 15:22

Yesu Kristo ni mtii na kondoo wake pia wanapaswa kuwa watii, Yesu Kristo alikubali kwanza kunyenyekea na kutii na kwenda msalabani na MUNGU akamwadhimisha na kumkirimia jina lipitalo majina yote. Wafilipi 2:5-10

Hivyo, Kristo ni kichwa cha kanisa Efeso 5:23-24 na sisi tu viungo vya Kristo 1Wakorintho 6:15 inatupasa kuwa na utii katika Kristo na kufanya mapenzi yake. Inatubidi tusikie sauti ya Yesu, Sauti ya Yesu ni neno la MUNGU, hivyo kila tunapojifunza katika neno, inatupasa kuliweka moyoni, ni lazima upende kulisikia neno la MUNGU, kulisoma neno la MUNGU na pindi neno linaposema badilika, yaani jambo lile ambalo Yesu anataka ulifanye katika neno lake lifanye mara moja na huko ndiko kumtii na kumfuata Yesu Kristo Yohana 10:27-28. Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata.  Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu.

UPENDO 1YOHANA 4:7-11


Upendo ndani ya Kanisa la kweli ni nguzo muhimu kwani MUNGU hukaa katika upendo, na upendo ni amri kuu ya Bwana Yesu, yeye MUNGU ni pendo na watu wote ndani ya Kanisa lake ni lazima wawe na upendo wa ndani, kuwapenda majirani na watu wote na pia kumpenda MUNGU. 1Wakorintho 13:1-13

No comments: