Ilikuwa suprise ya kipekee kwa Twi pale ambako hakutarajia kabisa tulimwimbia happy birthday kila mtu kwa lugha yake sijui kama hii imewahi kutokea unaweza ukawa umesherehekea sikuuuzako za kuzaliwa ila hii sidhani kama imewahi kutokea hogera Twilumba kwa kuongeza miaka kadhaa Sweety Mungu akupe maisha marefu mpaka kufika ile miaka ya ahadi .Na napenda kukuambia maneno haya nilikaa nikafikiri sana kabla ya kupost kwa blog ni maneno gani ya busara naweza kunena juu yako ili yakujenge kiroho na kimwili nikagundua nina hakiba na Hazina kubwa kwa baba yangu na siyo vyema nikisema happy birthday bila kusema kwamba kumcha Mungu na kuridhika ni faida kubwa. Kwa maana hatukuja na kitu cho chote hapa duniani, wala hatuwezi kutoka na kitu. Lakini kama tuna chakula na mavazi, basi tutaridhika. Watu wanaotamani kuwa matajiri huanguka katika majaribu na mtego na katika tamaa nyingi mbaya na za kijinga, ambazo huwato komeza wanadamu katika upotevu na maangamizi. Maana kupenda fedha ni chanzo cha uovu wote. Tamaa ya fedha imewafanya wengine watangetange mbali na imani na kuteseka kwa huzuni nyingi.Lakini wewe mtu wa Mungu, epuka haya yote. Tafuta kupata haki, utauwa, imani, upendo, subira na upole. Pigana ile vita njema ya imani. Shikilia uzima wa milele ulioitiwa ulipokiri lile ungamo lako jema mbele ya mashahidi wengine Mungu akubariki sana na hakupe hekima na upendo na watu wote
|
| | | | | | |
Twi hakimlisha Dada Lidya Keki
Ha ha ha h ah Rm S queer alipata naye keki kutoka kwa Dada Twi
Nahisi kizungu zungu ila presha imeshuka Chef wetu mkuu Maura naye alilishwa kwa style ya aina yake
Tamuuuuuuuuuu keki tamuuuuu
Life has got to be lived - that's all there is to it. At seventy, I would say the advantage is that you take life more calmly. You know that 'this, too, shall pass!'
No comments:
Post a Comment